Burudani

Diamond athibitisha kuwa kuna kinywaji wanaingia nacho mkataba kwa ajili ya Wasafi Festival, Inawezekana ni Mo Faya ya Alikiba ?

Diamond athibitisha kuwa kuna kinywaji wanaingia nacho mkataba kwa ajili ya Wasafi Festival, Inawezekana ni Mo Faya ya Alikiba ?

Msanii wa muziki wa kizazi kipya na C.E.O wa lebo ya muziki ya Wasafi pamoja na Wasafi Tv na Wasafi Fm Diamond Platnumz amethibitisha kuwa kuna kinywaji tayari wataingia nacho mkataba kwa ajili ya tamasha la Wasafi Festival.

Kupitia Ukurasa wake wa Twitter Diamond ameandia maneno hayo na kusema “Management imenambia kuna Kinywaji kesho kinaingia Rasmi onboard kama Mdhamini Mkuu wa …Labda nikitaarifu tu kuwa kijiandae kutengeneza Storck za kutosha maana sio tu kunywewa, bali hata wengine watataka kukiogea kwa promo ntayokipa…. “

Wengi wamekuwa wakitafsiri kauli hii kuwa huenda ni kinywaji cha Mofaya ambacho kipo chini ya msanii mwenzake kutoka Tanzania Ally Kiba kwani siku za hivi karibuni Diamond alimuomba Ali kushiriki katika tamasha lake la Wasafi Festival na Kiba kumwambia kuwa ” Kutokana na majukumu aliyonayo ya kuisambaza Mofaya hatoweza kushiriki labda ampe sapota kwa ajili ya kudhamini tamasha hilo kwa kinywaji chake cha Mofaya”

Na baada ya muda Diamond alimjibu na kusema kuwa uongozi wake ukiongozwa na Sallam Sk tayari umeanza mazungumzo na meneja wa Kiba Seven Mosha, Baada ya muda tena Sallam alithibitisha ni kweli wamekutana na Mosha na mendeleo ya kikao chao hayakuwa mabaya.

Na baada ya yote kauli ya Diamond ndio hiyo.

By Ally Juma.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents