Burudani

Diamond atuonjesha kionjo cha ngoma yake mpya aliyomshirikisha Lil Wayne

Diamond atuonjesha kionjo cha ngoma yake mpya aliyomshirikisha Lil Wayne

Msanii wa Bongo Fleva Diamond Pltnumz ameamua kutuonjesha kionjo cha ngoma yake aliyomshirikisha msanii kutoka Marekani Lil wayne.

Hapo nyuma meneja wake Sallam Sk wakati anafanyiwa mahojiano na kituo cha habri cha Times Fm alifunguka na kusema kuwa kuna kitu kizuri kinakuja baada ya kuulizwa swali juu ya kolabo ya msanii wake ambaye ni Diamond na msanii wa nje na kusema kuwa kuna kolabo inakuja akiwa amefanya na Lil Wayne.

Mapema jana msanii huyo ameweza kutuonjesha kionjo hicho huku akionekana yuko studio na wasanii wenzake kutoka katika lebo hiyo ya WCB Wasafi.

Baada ya yeye kupost kionjo hicho kwenye Insta story yake lakini pia msanii mwingine kutoka WCB wasafi Harmonize aliweza kupost kionjo hicho pia kwenye insta stori yake.

Diamond licha ya kufanya kolabo kadhaa kutoka nje ya nchini mfano Nigeria na nchini nyinginezo kutoka Afrika lakini pia msanii huyo amewahi kufanya ngoma na wasanii kutoka Marekani wakiwemo Neyo nyimbo inayojulikana kama Marry you, Rick Ross ngoma ya Waka waka na Omario ngoma ya African Beauty lakini pia ngoma ya Halleluyah akifanya na kundi la Morgan.

 

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents