Burudani

Diamond azidi kuangukiwa na neema za mastaa wa Marekani

Milango ya ustaa inazidi kufunguliwa kwa Diamond Platnumz.

Msanii huyo kutoka WCB ameonekana kuanza kuwateka mastaa wakubwa Marekani. Baada ya Dj Khaled kumfollow na rapper Rick Ross kumpost hitmaker huyo wa Eneka kwenye mtandao wa Instagram, Swizz Beatz na yeye ameamua kufuata nyayo kama hizo.

Swizz ameonekana katika kipande ha video akimtaja Diamond. Hata hivyo haikuishia hapo producer huyo ambaye pia ni mume wa msanii Alicia Keys ame-comment katika video hiyo ambayo Diamond ameipost katika mtandao huo.

“@diamondplatnumz Bless up King????????????,” ameandika Beatz katika video hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents