Burudani
Diamond Kuponea kuungwa miezi 6!
Habari zilizotufikia B5 ni kwamba Msanii wa kizazi kipya anayetawala kimuziki muda huu,
na maarufu pia kwa uhusiano wake na Miss Tanzania aliyepita Wema Sepetu, amehukumiwa kufungwa miezi sita au kulipia faini ya elfu hamsini, kufuatia kumpiga na kumuumiza mwandishi wa habari huko alikokua anafanya show ya mwaka mpya.
Taarifa zilizotufikia ni kwamba Diamond alipandishwa kizimbani baada ya kutokubali kumuomba msamaha mwandishi huyo ambaye amekiri kuumizwa na kuvunjiwa vifaa vya kazi pale ambapo Diamond alipompiga na kumjeruhi.
Marafiki wa karibu wa Diamond wamesema msanii huyo atalipa faini hiyo pamoja na kumfidia mwandishi aliyemshtaki ili aweze kununua vifaa vyake vya kazi