Diamond Platnumz
Diamond Platnumz kufanya show mbili kwa mpigo usiku wa leo – Geita na Mwanza
Hii ni sababu nyingine kubwa ya kuamini maneno yetu kwenye orodha ya wasanii wa Bongo Flava walioingiza fedha nyingi zaidi mwaka huu kuwa kila wiki Diamond Platnumz ambaye amekamata nafasi ya kwanza huingiza shilingi milioni 40.
Usiku wa kuamkia leo alikuwa na show iliyofunga visiwani Zanzibar na leo usiku atakuwa na show mbili. Ataanza Geita na baadaye kwenda Rock City kwenye Serengeti Fiesta.
“GEITA..!!!!!! On Ma Way… tukutane wote Desire Park! Usiku wa Leo, kabla sijenda kuvunja Jukwaa la Fiesta usiku huu huu wa leo kwenye viwanja vya CCM Kirumba Mwanza….! #OneNight #TwoShows #UsiulizeNafikajeWeNiachieMimi,” ameandika Staa huyo wa Number 1 kupitia Instagram.
Talking good money!!