Burudani
Diamond, Rayvanny wafungiwa na BASATA kufanya show ndani na nje ya nchi, Wasafi Festival yapigwa STOP kuendelea (+audio)
Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limewafungia wanamuziki wa Bongo Fleva kutoka WCB, Diamond Platnumz na Rayvanny kutofanya show ndani na nje ya nchi kwa muda usiojulikana.
Taarifa iliyotolewa leo Desemba 18, 2018 na BASATA, imesema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya wasanii hao kuonyesha dharau kwa mamlaka zinazosimamia shughuli za sanaa nchini, kwa kufanya vitendo vinavyokiuka maadili.
Kwa upande mwingine, BASATA wamefuta kibali cha Tamasha la Wasafi Festival linalotarajiwa kufanyika nje ya nchi baada ya kuzunguuka kwenye baadhi ya mikoa hapa Tanzania.
Imeelezwa kuwa wimbo wa Mwanza ndio uliowaingiza matatani, baada ya wasanii hao wikiendi iliyopita kuonekana jukwaani katika Tamasha la Wasafi Festival jijini Mwanza wakitumbuiza wimbo huo.