Burudani

Diddy azidi kuwatoa jasho mastaa wa Hip Hop duniani

Sean ‘Diddy’ Combs ni kama mwanga kwenye giza. Rapper huyo ametajwa kuongoza orodha ya mastaa wa Hip Hop waliolipwa fedha nyingi mwaka huu, hilo ni kwa mujibu wa jarida a Forbes.

Rapper huyo ametajwa kulipwa kiasi cha dola milioni 130 kwa miezi 12 iliyopita. Drake anafuata kwenye orodha hiyo akiwa amelipwa dola milioni 94.

Wakati huo huo Jay Z ambaye orodha iliyopita alishika namba mbili ameporomoka mpaka katika nafasi ya tatu akiwa amelipwa dola milioni 42 kwa mwaka huu. Hii ni orodha ya mastaa 10 walioongoza kulipwa zaidi.

1. Diddy
2. Drake
3. JAY-Z
4. Dr. Dre
5. Chance the Rapper
6. Kendrick Lamar
7. Wiz Khalifa
8. Pitbull
9. DJ Khaled
10. Future

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents