Habari

Didier Drogba kuondoka Chelsea kuenda China

Chelsea FC imedhibitisha kwamba star wao aliyefunga goli la kutwaa ubingwa juzi,Didier Drogba atakua akiondoka Chelsea pindi mkataba wake ukiisha mwezi wa sita mwaka huu.

habari hizo zimewaikitisha mashabiki wa timu hiyo lakini club imetoa tamko la kwmba ingawa hawatapenda kumuona Drogba akiondoka watajitahidi kuendelea kuwa timu bora katika mchezo wa mpira wa miguu.

Drogba mpaka sasa hajazungumzia kuhusu issue ya kuondoka ila wadau wake wa karibu wamesema kuna ishara kana kwamba atahamia kwenye club ya mpira iliyopo China iitwayo Shanghai Shenhua.

Drogba ataungana na mchezaji mwenzie wa zamani Nicholas Anelka ambapo atalipwa £250,000 kwa wiki.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents