Burudani
Diva wa Clouds kurekodi wimbo na ‘King wa Rap’ Collo wa Kenya
Mtangazaji wa Ala za Roho ya Clouds Fm na msanii wa bongo fleva Diva Loveness Love anatarajia kufanya collabo na mmoja wa malegend wa hip hop ya Kenya King wa Rap Collo.
Kupitia Instagram Diva aliweka picha ya Collo na kuandika “so Excited tell you guys Ntafanya Kazi Moja na @Collo_ King ….. and as you know mie shabiki wake wa Nyimbo alioimba na STL stella Mwangi Floss na wewe. check it on youtube. fan toka Enzi za Kleptomaniax…… Sooo Humbled, honored and Excited”.
Hivi karibuni Collo alikuja Tanzania na kufanya collabo na wasanii kadhaa akiwemo Diamond Platnumz, na kwa bahati mbaya wiki iliyopita King wa Rap alipata msiba kwa kuondokewa na baba yake.