Burudani
DJ D-Ommy wa Times FM ahamia Clouds FM
Aliyekuwa DJ wa vipindi vya Times FM kama vile ‘The Jump Off’ na ‘The Switch’, D-Ommy, amejiunga na Clouds FM.
D-Ommy amesikika kwa mara ya kwanza Alhamis hii baada ya kutambulishwa kwa surprise kwenye kipindi cha XXL.
Pamoja na kuwa DJ wa redioni, D-Ommy anafahamika kwa kujituma na kujitangaza katika kazi hiyo ikiwa ni pamoja na kutengeneza mixx tape za mbalimbali na kusafiri katika nchi za jirani kwenda kujitangaza.
D-Ommy akiwa na wafanyakazi wa Clouds Media, Adam Mchomvu, Nickson George na Kamara
D-Ommy amejichukulia pia umaarufu kwenye show za Instagram Party.