Burudani
Dj Khaled atangaza ujio wa albamu yake ya 11 ‘Father of Asahd’
Dj Khaled anampango wa kuachia albamu yake mpya hivi karibuni.
Rapper huyo amethibitisha hilo kupitia mitandao yake ya kijamii wakati akitambulisha kuachia ngoma yake mpya Ijumaa hii ya March 2.
Albamu hiyo itakuwa ya 11 kwa Khaled na tayari ameipa jina la ‘Father of Asahd’ ambalo linatokana na mwanae mwenye mwaka 1 na miezi minne.
#TopOff 🔝🚀 @djkhaled Featuring #JayZ @1future @beyonce Available Every Where Friday 6am Eastern 3am Pacific pic.twitter.com/KFnGVizSOC
— DJ KHALED (@djkhaled) March 2, 2018
Wimbo ambao Dj Khaled anatarajiwa kuuachia Ijumaa hii unaitwa ‘Top Off’ ambao amemshirikisha Jay Z, Beyonce na rapper Future.