Burudani
Dj Khaled azidi kutayarisha silaha za ‘Grateful’
Dj Khaled ameendelea kuviteka vichwa vya habari duniani ikiwa ni siku chache zimebakia kabla hajaachia albamu yake mpya ‘Grateful’.
Baada ya kumalizana na Rihanna kushoot video ya wimbo wake mpya ambao utapatikana katika albamu hiyo, Khaled ameingia tena location kutengeneza video ya wimbo wake aliomshirikisha Nas na Travis Scott.
“MORE HISTORY! BE READY!! @nas #djkhaled #GRATEFUL #JUNE23rd FAN LUV PRE ORDER NOW ON @itunes … LION ? ORDER ! GOD IS THE GREATEST!,” AMEANDIKA Khaled kwenye moja ya picha alizoziweka katika mtandao wa Instagram.
Albamu ya ‘Grateful’ itaanza kupatikana Juni 23 ya mwaka huu, lakini pia imeshaanza kupatikana kama pre order.