DJ wa kike na mtoto wa bilionea wa Nigeria, DJ Cuppy kutua Dar wiki hii
DJ wa kike wa Nigeria na mtoto wa bilionea wa nchini humo, Femi Otedola, aitwaye DJ Cuppy anatua Dar es Salaam wiki hii. Mrembo huyo ambaye anakuja Dar akitokea Nairobi, Kenya yupo kwenye ziara ya kuzunguka nchi takriban nane za Afrika.
Cuppy atatumbuiza Dar, Jumamosi hii.
Mfahamu zaidi Cuppy na baba yake bilionea, Otedola.
Femi Otedola ni CEO wa kampuni ya mafuta ya Forte Oil Plc mwenye utajiri wa dola bilioni 1.2. Otedola ana watoto watatu wa kike akiwemo Florence Otedola maarufu kama DJ Cuppy ambaye hufanya kazi ya UDJ jijini London Uingereza.
DJ Cuppy akiwa kazini
Mwaka huu, DJ Cuppy ndiye aliyekuwa DJ rasmi kwenye tuzo za MTV MAMA jijini Durban, Afrika Kusini. Yaani yeye ndiye alikuwa akipiga muziki wakati wa tuzo hizo.
Chini ni baadhi ya picha za DJ Cuppy akiwa na baba yake.