Michezo

Djokovic ajiwekea historia mpya, sasa alingana na Pete Sampras kwa mataji

Msimu wa majira ya joto umekuwa mzuri mno kwa mchezaji tennis, Novak Djokovic baada ya kukamilisha safari yake ya kutwaa taji la pili kubwa Grand Slam usiku wa kuamkia leo Jumatatu katika dimba la Arthur Ashe.

Djokovic kisses the trophy after getting through a contest that rarely troubled him in three hours and 16 minutes of play

Mserbia huyo mwenye umri wa miaka 31, amefanikiwa kumshinda, Juan Martin Del Potro kwenye michuano ya US Open kwa jumla ya seti 6-3, 7-6 (7-4), 6-3 na kutwaa ubingwa huo.

Kutokana na matokeo hayo, Djokovic anashika nafasi ya nne katika viwango vya ubora wa mchezo huo huku kukiwa na uwezekano wa kufika hadi nafasi ya kwanza mwishoni mwa mwaka huu.

Novak Djokovic holds the US Open men's singles trophy after beating Juan Martin del Potro 6-3, 7-6 (7-4), 6-3 on Sunday

Baada ya kushindwa kunyakua taji hilo kwa hisia kali kabisa, Del Potro amesema kuwa si rahisi kwa yeye kulizungumzia hilo.

”Si rahisi kulizungumazia swala hilo ila najiskia faraja kufika hatua ya fainali na kucheza na mchezaji huyu hatari kwa sasa. Najiskia huzuni kupoteza lakini najua ni furaha kwa Novak na anastahili,” amesema Del Potro.

”Sikuweza kukata tamaa kutokana na matatizo yangu, nilijaribu kucheza hatakama nilikuwa na majeraha nimefanikiwa kufika hapa leo hatua ya fainali na najivunia kwa hilo.”

Kwa Djokovic hili ni taji la 14 na anafahamu mbinu mbalimbali za namna ya kushinda haswa anapofika katika hatua ya fainali.

The agony and pain as Del Potro reacts during Sunday evening's US Open men's singles final at Flushing Meadows

Juan Martin Del Potro

Djokovic sasa yupo sawa na Pete Sampras kwakuwa na mataji 14 kila mmoja na kushinda pauni milioni 2.94.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents