Burudani

Documentary ya Chris Brown ‘Welcome To My Life’ kuachiwa mwezi Juni

Baada ya kusubiriwa kwa kipindi kirefu ujio wa documentary ya Chris Brown, imetajwa kutoka mwezi Juni mwaka huu.

Muimbaji huyo amethibitisha hilo kupitiaa mtandao wa Instagram, kwa kuweka video ya trailer ya documentary hiyo na kuandika, “In theaters ???? June.”

Documentary hiyo itakayoitwa ‘Welcome To My Life’ itakuwa ikizungumzia maisha ya muimbaji huyo aliyowahi kupitia, ikiwemo mahusiano yake na aliyewahi kuwa mpenzi wake Rihanna, yaliyomsababishia kuchukiwa na mashabiki baada ya kumshushia kipigo kizito.

Pia kwenye makala hiyo itakayowaonyesha mastaa waliowahi kufanya kazi na Chris akiwemo Jennifer Lopez, Usher, Mike Tyson, Jamie Fox na Rita Ora.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents