Dodoma: Wallace Karia rais mpya TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hatimaye limepata rais mpya ambaye ataliongoza kwa muda wa miaka minne kabla ya kufanyika tena uchaguzi Mkuu.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wakili msomi, Revocatus Kuuli amemtangaza, Wallace Karia kuwa rais mpya wa TFF baada ya kupata jumla ya kura tisini na tano huku akiwaacha wapinzani wake mbali.
Katika matokeo hayo ya uchaguzi wajumbe wa TFF wamempitisha, Mulamu Nghambi kuwa makamu wa rais baada ya kupata jumla ya kura 25.
Hawa ndiyo baadhi ya wagombea na idadi ya kura walizo pata
URAIS
A: Wallace Karia amepata jumla ya kura 95
B: Fredrick Mwakalebela amepata kura 3
C: Emmanuel Kimbe amepata kura 1
D: Iman Madega amepata kura 8
E: Shija Richard amepata jumla ya kura 9
F: Ally Mayay amepata jumla ya kura 9
By Hamza Fumo