[youtube]http://www.youtube.com/watch?v=t69xYnd2AAc[/youtube]
Baadaya mwanamuziki Aslay Ismail Dogo Aslay kutikisa katika kundi la Mkubwa na Wanawe linaloongozwa na mkubwa Fella, hivi sasa dogo mpya anaibuka kwa jina la Dogo Mu katika kundi hilo. mwanamuziki huyo ambaye atakuwa mdogo kuliko Aslay na kundi zima la Mkubwa na Wanawe mwenye umri wa miaka kumi na nne, mwenyewe anasema anataka kuja kumfunika kaka yake huyo (Aslay) wa kundi moja, ambapo kwa sasa naye anafanya mazoezi ya ziada ili azibe nafasi yake isije ikarabwa na dogo huyo.
Hebu kwanza msikilize kwenye moja ya Verse zake, ambazo anakuja nazo kwenye wimbo wake mpya.