Burudani

Dogo Janja atimiza ndoto yake kwa kukutana na Alikiba

Msanii wa Bongo Flava kutoka kundi la Tip Top Connection, Dogo Janja hatimaye amefanikiwa kutimiza moja ya ndoto yake.

Dogo Janja anayehit na ngoma ya ‘Ngarenaro’ amefunguka hayo baada ya kukutana na mkali wa ngoma ya ‘Seduce Me’, Alikiba na kupiga naye picha.

“Alhamdulilah leo nimetimiza ndoto yangu ingine yakupiga picha na alikiba @officialalikiba #Ngarenaro Link In My Bio,” ameandika Jajaro baada ya kukutana na Alikiba jijini Arusha.

Alikiba na Dogo Janja ni moja ya wasanii watakoshambulia jukwaa la muziki la Fiesta linalotarajiwa kuanza rasmi katika Mkoa wa Arusha hapo kesho Jumamosi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents