Burudani

Dogo Janja atoa somo katika uvaaji wake

Msanii wa Bongo Flava, Dogo Janja ametoa soma katika uvaaji wake.

Rapper huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Ukiavaaje Unapendeza’, ameimbia Dj Show ya Radio One kuwa watu wengi wamekuwa wakidhani ili mtu apendeze ni lazima awe na fedha nyingi kitu ambacho si kweli.

“Watu wamekuwa wakilinganisha muonekano wangu na fedha, ninachoamini kuvaa sio fedha nyingi sana ila kuvaa ni passion ya mtu, so kila mtu anavaa ndio maana nikasema ukivaje unapendeza kitu ambacho kipo watu wanavaa huwezi kutembea utupu hata siku moja,” amesem Dogo Janja.

Kabla ya kuachia ngoma yake “Ukivaje Unapendeza’ aliingia katika ubishani na watu wengi baada ya kujigamba kuwa yeye ndiye masanii anayeongoza kwa kupendeza Bongo.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents