Dongo la Mourinho kwa Pogba kabla ya kuivaa Arsenal ‘Hakuna nafasi kwa watu wasiyokuwa tayari kujitolea’
Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho ameonekana kuhoji uwajibikaji wa Paul Pogba wakati wakijiandaa kuwakabili Arsenal usiku wajana siku ya Jumatano.
Pogba hakuwa sehemu ya kikosi cha kwanza cha Mourinho wakati walipokuwa wakiikabili Arsenal na badala yake akitokea benchi.
”Hakuna nafasi kwa watu ambao hawapo tayari kujitolea,” Mreno huyo aliandika maoni yake wakati wa maandalizi wa mechi hiyo.
”Ni lazima tuwe imara, wenye kujiamini na kuwa wamoja kujenga imani kwa mashabiki zetu.” Mourinho alithibitisha hilo baada ya kufanya maamuzi ya kumuacha, Pogba.
Mourinho na Pogba wamekuwa na kutokuwa na mahusiano mazuri tangu kuanza kwa msimu huku ikiripotiwa kuwa kiungo huyoaliandika ujumbe na kuusambaza kwenye vyumba vya wachezaji vya kubadilishia nguo baada ya kutoka sare ya mabao 2 – 2 dhidi ya Southampton wikiendi iliyopita.
Mwanzoni mwa msimu Pogba alimtupia lawama Mourinho kwa aina ya mchezo wake na kusema lazima timu icheze kwa kushambulia zaidi.