Michezo
Dortmund yathibitisha mchezaji wake kwenda Manchester United
Timu ya Borussia Dortmund imethibitisha kuwa mchezaji wake Henrikh Mkhitaryan anakwenda Manchester United.
Kupitia akaunti ya Twitter, timu hiyo imeandika ujumbe unaoeleza kuwa mchezaji huyo anaelekea United kutokana na kukubaliana kwa masharti ya kumsajili. Manchester United inatajwa kuwa imetumia paundi milioni 26 kuishawishi Dortmund ili kumwachia mchezaji huyo raia wa Armenia na kumfanya kuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa chini ya kocha Jose Mourinho.
Mkhitaryan amefanikiwa kuichezea timu ya Dortmund jumla ya mechi 88 na kufunga magoli 23.