Burudani
Drake Kuibwa na Jay Z?
Tetesi zimeenea kwamba Rapper Superstar Drake aka Drizzy kutoka kwenye kundi la Young Money Cash Money billionaires, linalomilikiwa na Baby, ana mipango ya kuihama kundi hilo ambalo alitambulishwa rasmi na Lil Wayne, na kuingia katika mkataba na Roc Nation iliyopo chini ya usimamizi wa Jay Z.
Habari hizo zilizoenea kwenye ulimwengu wa rap zinasema kwamba Baby aliyedai kuwa Lili Wayne ni rapper bora zaidi ya Jay, aliona kama tishio kutoka kwa Jay baada ya kuenea habari za Drake kuachana na young Money, na kukanusha madai hayo.
Drake alitoa tamko kupitia XXL Mag ya Marekani na kusema kwamba yeye yuko katika mkataba na Aspire Young Money Cash Money na hana mpango wa kuihama label hiyo