Habari
Dudu Baya aokoka rasmi, Amshukuru Mtume Boniface Mwamposa kwa kumpa maisha mapya (+Picha)
Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Godfrey Tumaini almaarufu Dudu Baya leo Jumapili Agosti 25, 2019 ameokoka rasmi kwa kufanyiwa ibada na Mtume Boniface Mwamposa ‘Bull Dozer’ wa Kanisa la Inuka Uangaze Kawe jijini Dar es Salaam.
Dudu Baya akiongea mapema leo baada ya kumalizika kwa Ibada hiyo amesema “Kwasasa mimi ni mpya, Namshukuru sana Mwamposa kwa kwa kunipa neno la imani”.