Uncategorized
Dullah wa Planet Bongo afiwa na mtoto wake
Mtangazaji wa kipindi cha Planet Bongo kutoka East Africa Radio & TV Abdallah ‘Dullah’ Hamis Ambua wengi tunamjua kwa jina la Mjukuu wa Ambua jana amefiwa na mtoto wake wa kwanza, ambaye alikua na siku moja tu tangu kuivuta pumzi ya duniani…
Kwa mujibu wa taarifa toka kwa watu waliokaribu na msanii huyo mtoto huyo alifariki juzi na kuzikwa siku hiyo hiyo.
Bongo5.com inakupa pole kijana mwenzetu Abdallah, tuko nawe katika kipindi hiki kigumu kwako na familia yako. Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya mtoto huyo wa Abdallah..Amen