Dully Atoa Somo
Msanii Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ ametoa
somo kwa wasanii wachanga kuwa na nidhamu kwa watu wote ili wafikie
mafanikio katika kazi yao ya kimuziki
Ushauri huo ameutoa juzi
alipokuwa akizungumza kwenye kipindi cha mahojiano maalumu na
televisheni moja ya jijini Dar es Salaam.
“Napenda kuwaambia wasanii wachanga wakitaka kufika mbali hawana budi
kuwa na nidhamu katika kazi zao ili wafanikiwe,” alisema.
Dully alisema kwamba sababu ya yeye kuendelea kuwa juu ni nidhamu aliyo nayo kwa watu wote bila kujali ana uwezo gani.
“Nidhamu ndicho hasa kitu kilichoniwezesha kuendelea kuwa juu kila
siku, mara zote kwa watu wanaonijua nimekuwa si kawaida yangu kuacha
kutaniana nao au kuwasalimu,” alisema.