Burudani
Dully Sykes alia na wasanii waliomtenga kwenye msiba wa baba yake
Wanasema rafiki wa dhati utamjua wakati wa dhiki na tayari Dully Sykes amechuja marafiki wa kweli na feki.
Dully ambaye wiki hii alimzika baba yake, Mzee Ebby Sykes amesema hatopenda kuendelea kuwatupia lawama wasanii waliomtenga kwenye msiba huo na kwamba hilo anamuachia Mungu.
“Hili suala nilishaambiwa nisizungumze tena kuhusiana na msanii ambaye hajafika, kwahiyo namwachia mwenyezi Mungu,” ameiambia Bongo5.
“Sio tu kwa msanii ambaye hajadhuria wala kuniandikia meseji kwa sababu kuna baadhi ambao hawajafika lakini wako mbali na wameniandikia meseji lakini kuna wasanii ambao niko nao karibu hata meseji hawakuniandikia.”