Burudani

Ebitoke ajibu ishu ya kumsaliti Ben Pol na kutembea na Shemeji yake (+video)

Mchekeshaji kutoka kundi la Timamu, Ebitoke amejibu tetesi za kutoka kimapenzi na Wyse ambaye ni msanii anayesimamiwa na Ben Pol.

Ebitoke na Wyse

Utakumbuku kuwa Ebitoke na Ben Pol kwa kipindi kirefu sasa wamekuwa wakieleza kuwa wao ni wapenzi hivyo, Wyse ni shemeji yake na Ebitoke.

Mchekeshaji huyo amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote kwani mapenzi yake na Ben Pol bado ni ya moto kabisa na picha zilizotoka wakiwa wana-kiss ni katika kutengeneza video ya Wyse.

“Director alituambia tu-kiss ili kuvaa uhalisia ila kati yangu na Wyse ni urafiki hakuna mapenzi,” Ebitoke ameiambia Bongo5.

Muimbaji Wyse anasimamiwa na Ben Pol na kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Siamini’, pia alishirikishwa na Ben Pol katika wimbo wake uitwao Bado Kidogo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents