Habari
EFM yakanusha kurusha habari ya Profesa Kitila kukataa uteuzi wa Rais Magufuli
Kituo cha redio cha EFM, kimekanusha taarifa zilisambaa mtandaoni kuwa Profesa Kitila Mkumbo aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji amekataa uteuzi huo. Kituo hicho kimesema taarifa hizo ni za uzushi.
Hii ni taarifa yake:
Wakati huo huo Profesa Mkumbu ametweet: Namshukuru mhe Rais @MagufuliJP kwa heshima aliyonipa katika kutumikia nchi yetu katika nafasi ya Katibu Mkuu. Mungu anisaidie.
Na Emmy Mwaipopo