Emmanuel Adebayor asajiliwa na Crystal Palace
Klabu ya Crystal Palace ya ligi kuu ya England imemsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Togo Emmanuel Adebayor.
Adebayor amesajiliwa na timu hiyo akiwa mchezaji huru kwa mkataba ambao utamuweka chini ya meneja Alan Pardew mpaka mwisho wa msimu huu wa ligi.
Mshambuliaji huyu mwenye umri wa 31 aliachwa na timu yake ya Tottenham mwezi Septemba mwaka jana, na amefunga jumla ya magoli 94 katika Ligi ya England akiwa amezichezea timu za Tottenham,Arsenal na Manchester City.
Mara ya mwisho kucheza mchezo wa ligi ilikua ni mwezi mei mwaka jana katika mchezo kati ya timu yake ya Tottenham na Man City .
Adebayor ambaye alijiunga na Arsenal, akitokea klabu ya Monaco, ya Ufaransa.baadae akajiunga na Man City kabla ya kupelekwa kwa mkopo kwa miamba wa soka wa Hispania Real Madrid na mwaka 2012 akajiunga na Tottenham.