Burudani

EXCLUSIVE: Binti Kiziwi amaliza kifungo cha kesi ya Madawa ya Kulevya China, uso kwa uso Dar na Z Anto (Video)

Video Queen, Sandra Khan maarufu kama ‘Binti Kiziwi’ amerejea kimya kimya nchini Tanzania Disemba 2019 baada ya kumaliza kifungo cha miaka 8 jela kwa kosa la kusafirisha madawa ya kulevya.

Mrembo huyo ambaye alifungwa Hong Kong China mwaka 2012 kwa kosa hilo, alimaliza kifungo chake Disemba mwaka 2019, na baada ya hapo alirudishwa nchini Tanzania.

Ijumaa hii muimbaji, Z Anto ambaye alimtambulisha mrembo huyo kwenye tasnia ya sanaa kupitia wimbo Binti Kiziwi, amlitembelea na kuzungumza naye mawili matatu kuhusu maisha yake mapya baada ya kurejea uraiani.

Bongo5 imezungumza kiundani na Binti huyo, Taarifa kamili inakuja.

 

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents