Exclusive; Feza Kessy na Ammy Nando ndio wawakilishi wa Tanzania kwenye BBA ‘The Chase’ (picha za airport wakielekea Bondeni)
Sasa tunaweza kuthibitisha kuwa Tanzania inawakilishwa na washiriki wawili kwenye shindano la mwaka huu la Big Brother Africa lililopewa jina la ‘The Chase’. Ufunguzi wa shindano hilo umeanza muda huu huko Afrika Kusini. Washiriki hao ni Feza Kessy na Ammy Nando.
Feza Kessy ambaye aliwahi kuwa Miss Dar City Centre, hivi karibuni aliingia rasmi kwenye muziki na kuachia single yake ya kwanza, Amani Ya Moyo. Yupo chini ya kampuni ya AY, Unity Entertainment. Hizi ni picha za Jumapili iliyopita aliposindikizwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es Salaam kuelekea Afrika Kusini. Siku hiyo Feza alisindikizwa na rafiki zake wakiwemo Vanessa Mdee na Leah Tsere.
Kwa upande wa Ammy Nando mwenye miaka 22, yeye muda mwingi alikuwa akiishi Los Angeles, California, nchini Marekani na ni model kwenye agency iitwayo Modelmayhem. Hizi ni picha zake.