Exclusive: Muigizaji wa Marekani, Meagan Good na mdogo wake Lamyia kuja Dar, December
Muigizaji wa filamu nchini Marekani Meagan Good na mdogo wake Lamyia Good wanatarajiwa kuja Dar es Salaam, mwezi December mwaka huu.
Kwa mujibu wa promoter wa kimataifa, Hemdee Kiwanuka ambaye pia ni meneja wa AY, ndugu hao warembo watakuja Dar kwenye party na dinner maalum kwaajili ya amani na umoja.
Meagan Good
“@AyTanzania….. Yo, @LamyiaGood and @MeaganGood are excited to come and support our Peace and Unity Dinner. We can’t wait. Are you ready?”Hemdee alitweet jana.
@bongofive Please push my artist… @AlphaRwirangira FT. @LamyiaGood http://t.co/GAWMw3On4S LaMyia will be in Dar in Dec w/ @MeaganGood
— hemdee kiwanuka (@hemdee31) September 22, 2013
@AyTanzania….. Yo, @LamyiaGood and @MeaganGood are excited to come and support our Peace and Unity Dinner. We can't wait. Are you ready?
— hemdee kiwanuka (@hemdee31) September 22, 2013
Meagan Good ni muigizaji maarufu aliyeigiza kwenye filamu nyingi za Hollywood zikiwemo, Friday, Waist Deep,Stomp the Yard, Jumping the Broom, Think Like a Man na zingine.
Pamoja na filamu, Good ameigiza kwenye series kibao za TV. Pia amewahi kuonekana kwenye video za muziki za wasanii kama 50 Cent, Lil’ Johnny, Memphis Bleek, Tyrese, na Will Smith.
Lamyia ni mwanamuziki aliyeshirikishwa na AY kwenye wimbo wake Speak With Ur Body.