Bongo5 MakalaBurudani
Exclusive: Nazizi aangukia tena kwenye penzi la Mtanzania, ni Sappy producer wa Home Boyz Productions (Picha)
Baada ya rapper wa Necessary Noize, Nazizi kuthibitisha kuwa ameachana na mume wake, Bongo5 inathibitisha kuwa rapper huyo kwa sasa ni mpenzi wa Mtanzania mwingine, Herry Sappy, mtayarishaji wa muziki kwenye studio ya Home Boyz Productions ya Kenya.
Penzi Motomoto: Sappy na Nazizi
Mume wa zamani wa rapper huyo ni Mtanzania pia.
Familia: Sappy na Nazizi wakimbusu mtoto wa rapper huyo
Sappy ameiambia Bongo5 kuwa uhusiano wake na Nazizi ulianza siku ya Valentine’s (Feb 14, 2014) na kwamba wapo serious na wanapenda kwa dhati.
“Mpango ni kuvishana pete,”Sappy ameiambia Bongo5.
Nazizi ana mtoto mmoja wa kiume aliyezaa na mume wake waliyeachana.