Burudani
FA atoa nafasi, wasanii kuchangia ajali ya meli
Nyota wa muziki wa kizazi kipya Mwana Fa, amesema kwakuwa ni mwenyekiti wa chama cha Wasanii Tanzania basi anatoa nafasi kwa mwaliko wowote kwaajili ya shughuli za kujitolea kuchangia na kusaidia waathirika wa ajali ya Meli ya Spice Islanders.
Anasema ingawa wasanii wachache wamekuwa wakiingia studio, lakini kama kundi bado kwakuwa hawajakutana kwaajili ya mchakato wa kujua wafanye nini katika suala hilo. hata hivyo amesema anakaribisha maombi kwa chama hicho, kwaajili ya shughuli yoyote ili kuonyesha wasanii wapo pamoja nao.