Habari

Fahamu upekee wa boti ya kisasa ya Kilimanjaro VII ya Bakhresa (Video)

Boti mpya ya Kilimanjaro VII inayomilikiwa na Bakhresa Group chini ya Azam Marine na Kilimanjaro Fast Ferries ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa hamu imewasili leo Zanzibar kutoka kiwandani Australia.

Boti hiyo itakayokuwa na huduma za kisasa zaidi hapa Tanzania, imefika Zanzibar ikiwa imebebwa juu ya meli maalum.

Kwa mujibu wa kampuni ya Azam Marine na Kilimanjaro Fast Ferries, boti hiyo inafanyiwa ukaguzi na kukamilisha taratibu nyingine za kimamlaka kabla ya kutangazwa muda wa kuanza huduma zake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents