Fally Ipupa anusurika kifo kwenye ajali ya gari huko Kinshasa
Mwanamuziki maarufu wa Congo Fally Ipupa, wiki hii amenusurika kifo baada ya gari aliyokuwa akisafiria kupata ajali huko mji mkuu wa DRC, Kinshasa.
Mwimbaji huyo kipenzi cha kinadada alitoka salama bila kuumia, huku taarifa zingine zikidai kuwa abiria mwenzake msichana ambaye hajafahamika alikimbizwa hospitali. Inasemekana kuwa Fally alikuwa akitokea studio wakati ajali hiyo ilipotokea Jumanne usiku.
Hii ni gari aliyopata nayo ajali Fally Ipupa
Baada ya ajali hiyo kumekuwepo na habari za uvumi mtandaoni kuwa mwanamuziki huyo ameumia sana, huku zingine zikidai kuwa amepoteza maisha kutokana na ajali hiyo, lakini Fally aliutumia ukurasa wake wa facebook kuweka sawa taarifa hizo.
“Mimi ni mzima…ni gari tu ndio imeharibika, Asante Mungu. Asanteni kwa meseji zenu.” Ameandika Fally.
Source: Standard Digital