Habari

Fat Joe anaweza kwenda jela miaka miwili kwa kukwepa kulipa kodi

Fat+Joe+Univision+Premio+Lo+Nuestro+La+Musica+ANd4jrqkOByl

Rapper Fat Joe ambaye aliwahi kutengeneza mkwanja wa nguvu kwa hits zake “What’s Luv” na “Make It Rain” amepatikana na hatia ya kukwepa kulipa kodi.

Rapper huyo mwenye miaka 42 ambaye jina lake halisi ni Joseph Cartagena anadaiwa na serikali kwa kutolipa kodi ya dola 700,000 kwa mwaka 2007 na 2008.

Joe alitokea mahakamani huko New Jersey kusikiliza kesi yake lakini yupo nje kwa dhamana ya dola 250,000. Hukumu yake itatolewa mwezi April mwakani na anaweza kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents