Michezo
FC Barcelona imekamilisha usajili wa Samuel Umtiti
Klabu ya FC Barcelona ya Hispania, imetangaza usajili wa mchezaji Samuel Umtiti kutoka klabu ya Olympique Lyonnais, Barcelona wametangaza kupitia tovuti yao.
Samuel Umtiti amesajiliwa kwa mkataba wa miaka mitano, kwa dau la uhamisho wa euro milioni 20, Umtiti ambaye anachezea timu ya taifa ya France alifanya vizuri katika mashindano ya Euro 2016 atakuwa akicheza nafasi ya beki wa kushoto au beki wa kati.