Ferooz alivyomtesa Adam
Mwanamuziki Feroozi akiwa pande za Temeke na Adam Juma katika kukamilisha video ya wimbo wake wa Mnanda, ambayo aliifanyia pande za Temeke aliweza kuvuta watu wengi kiasi cha mtengenezaji huyo wa video kuwa na wakati mgumu.. endelea kupata picha uone umati ulivyobana.
Kundi la akina dada waliokuwa wakizisumbua vyonga zao pale kati, kwaajili ya kuleta radha…
Hapa walikuwa wakijadiliana kidogo, akiwa Mkubwa Fella na Meneja wa Mkubwa na Wanawe Yusuph na Adam Juma.
Ilibidi muda mwingine Adam apande juu ya viti kupata picha nzuri, lakini bila hivyo ingekuwa balaa
Wengine walijisahau kabisa kama wapo kwenye Shooting, wakajikuta wakimwaga radhi..
Mwali…mwali.. hao wakawa wanakuja, wengine wakija na ndoo za maji ilimradi shangwe na nderemo….ilikuwa balaa tupu
Hapo sasa..Twende sasa…
Hapa sijui Muogo alikuwa akiwaza nini juu ya huyu Ngongoti, wakati Masawe akikoleza ngoma huku watishaji wakiwa pembeni na vinyago vyao… Big Up Adam kwa kujituma… Big Up mkubwa Fella kwa kuandaa michakato yote ya kuvutia…Big Up Feroozi kwa kutoa ngoma kama hiyo iliyochezeka hivyo.. Mwisho tunategemea Video kali itakayoendeleza muziki wetu wa Tanzania husasni Mnanda uliosahalika….
THE END