Burudani
Ferooz na Daz Baba hawajaonana kwa miaka minne!
Blame the city… Ferooz na Daz Baba hawajaonana kwa takriban miaka minne.
Akiongea kwenye kipindi cha Siz Kitaa, Daz Baba amesema mawasiliano pekee aliyoyafanya na member mwenzie huyo wa kundi la Daz Nundaz ni kwa simu.
Daz amedai kuwa uwezekano kwa kundi lao kurejea tena ni mgumu kwakuwa kuna wakati P-Funk alitaka kuwaunganisha tena lakini baadhi ya member hawakuonesha ushirikiano.
Naye Ferooz aliyehojiwa kwenye kipindi hicho cha Clouds TV hivi karibuni alidai kuwa kulirudisha kundi lao tena ni jambo linaloweza kufanyika lakini mpaka pale watakapopata menejimenti ya kusimamia kazi zao.