Burudani
Fid Q kufanya listening party ya album yake ‘Kitaaolojia’ Alhamis hii Nairobi, album itatoka July
Fareed Kubanda aka Fid Q Alhamis hii atafanya listening party ya album yake mpya, Kitaaolojia jijini Nairobi, Kenya.
Party hiyo itafanyika kupitia mradi wa Nairobi Rapsody kwenye kiota cha Ebony Lounge jijini humo.
Album hiyo itaingia sokoni mwezi ujao na itakuwa na nyimbo 10 zikiwemo Ielewe Mitaa, Neno aliyofanya na Lord Eyez, Sihitaji Marafiki aliyomshirikisha Yvonne Mwale kutoka Zambia, Siri ya Mchezo aliyomshirikisha Juma Nature, Bendera ya Chuma akiwa na Ben Pol na Bongo Hip Hop aliyomshirikisha P Funk Majani.
Pia kwenye album hiyo kutakuwepo na wimbo ambao Fid amewashirikisha Sauti Sol. Fid pia ni miongoni mwa wasanii waliopo kwenye msimu wa tatu wa Coke Studio Africa.