Burudani
Fid Style Friday ya Cheusi Dawa kurejea tena kwenye TV?
Inaonekana ile show ngumu na nyeusi zaidi kuliko zote kwenye TV za Tanzania, Fid Style Friday inaelekea kurudi tena hewani.
Show hiyo inayoandaliwa na kampuni ya Cheusi Dawa ya Fareed Kubanda aka Fid Q, ilikuwa imesimama kwa muda. Fid Style Friday ilikuwa ikiruka kupitia EATV na ilikuwa ikihusisha mahojiano na wasanii wa hip hop pamoja na kuchana mistari.
“The biggest hiphop show in Africa… ••••••• L O A D I N G ••••••• ,” ametweet Fid kuashiria kuwa ipo njiani kurejea tena.