Burudani

Fiesta ya Dar Es Salaam imepanga kuwapandisha wasanii hawa jukwaani (+Audio)

Fiesta ya Dar Es Salaam imepanga kuwapandisha wasanii hawa jukwaani

Katika kikomo cha Fiesta mwaka huu 2018 jijini Dar Es Salaam itakayofanyika jumamosi hii ya tarehe 24 mwezi wa 11 katika viwanja vya Leaders imepanga kuwapandisha wasanii wakongwe.

Akiongea kwenye kipindi cha Clouds Tv mmoja ya viongozi wakubwa katika kituo hicho Sebastian Maganga ameongea hayo, Maganga alisema:- KAMBI YA UPINZANI INATIKISA #TigoFiesta2018.
Sebastian Maganga amesema anatambua harakati za kambi ya Rasmi Upinzani ambayo kwa kiasi kikubwa imepanga kuwapandisha wasanii wakongwe pale Leaders Jumamosi hii. Ameeleza kwamba licha ya nguvu ya kambi hiyo, shughuli ni nzito kwa sababu vijana wa sasa hawako tayari kuona wakongwe hao wakiwashinda na hivyo Jumamosi shughuli itakuwa nzito Leaders.”

“Ajabu ni kwamba Seba naye hajui yuko kambi gani. Amesema “Uzuri mimi nimeshuhudia yote kizazi hiki pinzani kinachotaka kuhodhi madaraka, na kizazi hiki kipya kikiwa kinaanza. Mimi bado sijafanya maamuzi na pande zote zinanivutia na wanakazi kubwa.”

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents