Michezo
Floyd Mayweather asisitiza Andre Berto ni bondia wa mwisho kupigana naye
Bondia Floyd Mayweather amesisitiza kwa mara nyingine kuwa Andre Berto ndiye bondia wa mwisho kupigana naye katika pambano lao la Jumamosi.
Mayweather amesema watu wengi wanafikiri tofauti kwamba atapigana tena. Pambano hilo la 49 ndilo litakuwa la mwisho kwake na anataka kushinda kubaki na rekodi yake ya kutopigwa daima katika ngumi za kulipwa.
Andre Berto
Pambano hilo litafanyika Jumamosi katika Ukumbi wa MGM Grand Garden jijini Las Vegas, Marekani na tayari tiketi zimeanza kuuzwa na zinakaribia kuisha.