Promotion
Fuse ODG atweet kuhusu show yake ya Dar Sept 7, aahidi kuwasha moto
September 7 mwaka huu jiji la Dar es Salaam litachezeshwa mtindo maarufu wa uchezaji muziki wenye asili ya Ghana, Azonto na staa wa nchi hiyo aishie Uingereza, Fuse ODG.
Hitmaker huyo wa Azonto na Antenna anatarajia kufanya show hiyo kwenye viwanja vya Ustawi wa Jamii ambapo atasindikizwa na wasanii wa nyumbani wakiwemo Vannesa Mdee, Mabeste, Mrap, Deddy, Gosby, Wakazi, H Baba, Banana Zoro, Wakali Dancers, Lulu (BongoMovie), Aika na Nah Reel na wengine.
Leo msanii huyo ametweet:
TANZANIA… I'll be there on the 7TH SEPTEMBER in the main city Dar Es! We ready! AZONTO Tings…ANTENNA Buzz #TINA TZ let's go!
— ANTENNA OUT NOW (@FuseODG) August 28, 2013