Burudani
Future aweka wazi ratiba ya ziara yake mpya, aitaja Tanzania ndani yake
Rapper kutoka Marekani, Future ametangaza ujio wa ziara yake mpya ya muziki ambayo inaitwa ‘The Future Hndrxx Tour’.
Ziara hiyo inatarajiwa kuanza Julai 8 ya mwaka huu na kufikia tamati mjini London Oktoba 23, ambapo itazunguka karibia nchi kibao duniani ikiwemo kwenye bara la Marekani, Ulaya, Afrika na mengine.
Ratiba hiyo pia imeonyesha rapper huyo atatumbuiza katika jiji la Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Leaders Julai 22.
Ratiba ya ziara ya Future atakayozunguka dunia
Awali msanii huyo alitangaza ziara yake ya ‘Nobody Safe’ ambayo kwa sasa tayari ameshaipiga chini.