G-Nako, Adili, Salu T kuja na project ya ‘Shake the Industry’ nyimbo tano kuachiwa wiki hii
Studio mpya, jijini Dar es Salaam, B.Records kupitia producer wake Chizan Brain wiki hii inakuja project iliyopewa jina na G-Nako, Shake the Industry. Katika project hiyo, nyimbo tano zitaachiwa kwa pamoja wiki hii.
G-Nako
“Ntakuwa na five tracks watu tofauti project naiita ‘Shake the Industry’, Adili,Salu T, Henry,Nadyah,Gnako,” amesema GNako.
“Tracks tatu nimefanya nao collabo then Henry na Salu T wamefanya wenyewe bt zote studio Moja B.RECS CHINI YA CHIZANI BRAIN. Jumatano zinatoka zote na ndio maana naiita Shake the Industry.Ni Nyimbo tano zinazotoka kwa pamoja zenye maudhui tofauti,zenye vichwa vipya,zenye manguli wa hip hop studio mpya. Na pia kuna reggae, hip hop,afropop. On top of it production wise and mziki mzuri Kwa ujumla so hii itaamsha Ari mpya ya wanamuziki kutulia na kutengeneza mziki mzuri.”
Msikilize zaidi hapa: