Kampuni ya ulinzi ya G4s ikishirikiana na mradi wa kukuza mchezo wa Rugby kwa nchi za Afrika,leo wameendesha kliniki ya mafunzo kwa watotoa shule za msingi katika viwanja vya shule ya kimataifa Tanganyika.
kliniki hiyo iliongozwa baadhi ya wakufunzi kama Ryan Jones wa Afrika kusini Springboks,Juan Pablo,GUllaume Boisseau,Ben Illingworth,Jonathan Markiwitz and Mike Googan,katika kliniki hiyo watoto wa shule ya Tanganyka International School,Mapambano na Shekilango walijifuzwa ya awali ya mchezo huo kwa masaa mawili kabla ya kupewa ujuzi wa vitenndo kwa lisaa hilo moja katika maeneo ya kucheza salama,kuzuia na matumizi ya maji na namna bora ya kucheza kitimu.
Akiongea na bongo5.com mkurugenzi wa kampuni ya G4s ambao ndiyo wadhamini wakuu wa project hiyo alisema “Wao kama kampuni kubwa ya ulinzi wamejitolea kukuza mchezo huo kama sehemu ya kurudisha fadhila kwa jamii kwa miaka miwili wamekuwa wakidhamini na kusaidia programu mbalimbali ili kuakikisha mchezo huo unawajenga watoto kiafya,ukakamavu,na kujiamiani na pia unaweza usaidia kufufua vipaji ambavyo atuvijiui kama vipo kwaiyo kwakupitia kliniki hizi za mara kwa mara tutawasaidia watoto.”