Burudani

Gabo akanusha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Faiza Ally

Msanii wa filamu Gabo Zigamba, amefunguka kwa kusema kuwa hana mahusiano yoyote na msanii mwenzake wa kiwanda cha filamu Bongo, Faiza Ally.

12530671_535455813301660_231741592_n

Muigizaji huyo ambaye hivi karibuni amefanikiwa kushinda tuzo ya mwigizaji bora wa kiume kwenye tamasha la Ziff 2016, ameiambia Times FM kuwa hakuna mahusiano yoyote ya kimapenzi yatakayotokea kati yake na Faiza.

“Faiza namjua kama producer wangu, amenishirikisha kwenye filamu yake ya Baby Mama Drama. Hakuna chochote wala hayatotokea mahusiano ya kimapenzi kati yetu,” amesema Gabo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents