Bongo Movie
Gabo asema filamu yake mpya ya ‘Safari ya Gwalu’ italeta mapinduzi
Msanii wa filamu aliyetamba kwenye Bado Natafuta, Gabo Zigamba amesema filamu yake mpya ‘Safari ya Gwalu’ italeta mapinduzi nchini.
Gabo ameiambia Bongo5 leo kuwa uwezo aliouonesha katika kazi hiyo utawafanya watu waamini kipaji chake.
“Mimi nategemea mafanikio makubwa kwa sababu hii ni miba ya nyikani na haivunjiki kwa mkono,” amesema. Ajira isiyo rasmi sasa tunakwenda kuirasimisha, lazima nifanye vitu ambavyo vitaleta mapinduzi na changamoto kwa wengine. Safari ya Gwalu ni filamu inayokwenda kuishi kwa muda mrefu kwa sababu ni sinema ambayo itarudisha safari ya Gabo.”
Amesema filamu hiyo itatoka September 28.